Mkuu wa Idara Masoko wa Stanbic Bank Tanzania, Neemarose Singo, ametajwa kuwa miongoni mwa Viongozi 100 Bora wa Masoko Barani Afrika katika tuzo za kwanza za Africa CMO 100, mpango wa Brand Africa na washirika wake unaotambua viongozi wanaochagiza mikakati ya chapa, uelewa wa wateja na ukuaji wa biashara barani. 

Kwa mujibu wa Stanbic Bank Tanzania, utambuzi huu hauakisi tu uongozi wake binafsi bali pia ubora wa vipaji vinavyojenga taasisi hiyo kila siku. 

Benki hiyo imeeleza kujivunia kuwa makao ya watu wanaoleta matokeo, kujenga chapa zenye maana na kuchangia hadithi ya ukuaji wa Afrika, ikisisitiza kuwa taasisi kubwa hujengwa na watu wa kipekee.

Hongera sana Neemarose! 👏🏽